1 Corinthians 7:7-9
7 aLaiti watu wangekuwa kama mimi nilivyo. Lakini kila mtu amepewa kipawa chake kutoka kwa Mungu, mmoja ana kipawa cha namna hii na mwingine ana cha namna ile. 8 bKwa wale wasiooa na kwa wajane, nasema hivi, ingekuwa vizuri wasioe. 9 cLakini kama hawawezi kujizuia, basi waoe na kuolewa, kwa maana ni afadhali kuoa au kuolewa kuliko kuwaka tamaa.
Copyright information for
SwhKC